No link

Kuhusu Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa

Tangu kuanzishwa kwake katika mwaka wa 1972, Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) ni mamlaka ya kimataifa inayoweka ajenda ya mazingira, linawezesha utekelezaji wa vipengele vya mazingira vya maendeleo endelevu kwenye mfumo wa Umoja wa Mataifa, na hufanya kazi kama mtetezi mkuu wa mazingira duniani.

Dhima ya UNEP ni  kutoa uongozi na kuwezesha ushirikiano  wa kutunza mazingira kwa kuhimiza, kuelimisha na kuwezesha mataifa na watu kuimarisha maisha yao bila kuathiri yale ya vizazi vijavyo.

UNEP inafanya kazi ilikuleta mabadiliko chanya kwa watu na mazingira kwa kuangazia chanzo cha changamoto tatu duniani za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira na uharibifu wa bayoanuai, na uchafuzi na taka. UNEP inatumia programu ndogo saba zilizoingiliana kuchukua hatua: Kushughulikia MazingiraKushughulikia Kemikali na UchafuziKushughulikia Asili, Sera ya Sayansi, Kusimamia MazingiraMabadiliko ya Kifedha na Kiuchumi na Mabadiliko ya Kidijitali. 

Kupitia kampeni zake, hususan Siku ya Mazingira Duniani, UNEP huhamasisha na kupigania ushughulikiaji mwafaka wa mazingira.

Na Makao Makuu yake mjini Nairobi nchini Kenya, UNEP hufanya kazi kupitia kwenye idara zake na pia kupitia katika ofisi  zake za kikanda na kupitia kwa mtandao unaokua wa vituo vinavyoshirikia bora zaidi.

UNEP inafanya kwa ushirikiano na Nchi Wanachama 193 na wawakilishi kutoka mashirika ya kiraia, mashika ya biashara, na makundi mengine makuu na washikadau kushughulikia changamoto za mazingira kupitia Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa, taasisi ya ngazi ya juu zaidi inayofanya maamuzi duniani kuhusu mazingira.

Shirika hili ni mwenyeji wa sekretarieti za mikataba mingi muhimu kuhusu mazingira na mashirika ya utafiti.

Mkurugenzi Mtendaji na Kikosi cha Wasimamizi Wakuu wanaongoza utekelezaji wa Mkakati wa Muda (MTS) wa UNEP. MTS ya miaka minne inaelezea wajibu wa UNEP katika kutekeleza ahadi za Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu na Kongamano la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Endelevu (Rio+20) pamoja na hati ya matokeo yake, “Hatima Tunayoitaka.”

UNEP husaidia Nchi Wanachama kuhakikisha kwamba zinajumuisha uendelevu wa mazingira katika mipango ya maendeleo na uwekezaji na hutoa kwa nchi zana na teknolojia muhimu za kutunza na kuboresha mazingira. Kazi yake hufanikishwa na wabia wanaofadhili na kutetea dhima yetu. UNEP inategemea michango kutoka kwa wahisani kwa asili mia 95 ya mapato yake.

 

Ufadhili wetu

Fahamu tunakotoa fedha, tunavyozitumia, na jinsi tunavyoweza kuendesha miradi yetu vizuri kwa kuzitumia. 

Jifahamishe zaidi

 

Wasiliana Nasi

United Nations Avenue, Gigiri
Sanduku la Posta 30552, 00100
Nairobi, Kenya

Simu: +254 (0)20 762 1234
Barua Pepe: unenvironment-info[at]un.org
Mawasiliano na vyombo vya habari: unenvironment-newsdesk[at]un.org